Header Ads Widget

Mpina Aibuka Tena: Rejesha Fomu za Urais ACT-Wazalendo Dodoma Baada ya Ushindi Mahakamani

 



Dodoma, Septemba 13, 2025 – Mgombea urais wa Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Joelson Mpina, leo amerejesha rasmi fomu yake ya kugombea urais katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) zilizopo jijini Dodoma, hatua inayomrudisha rasmi kwenye mbio za Ikulu baada ya maamuzi ya Mahakama Kuu wiki hii.


Mpina aliwasili akiwa ameambatana na mgombea mwenza wake Fatma Ferej, huku akipokelewa na viongozi waandamizi wa chama hicho akiwemo Kiongozi wa Chama Dorothy Semu, Mwanasheria Mkuu wa ACT-Wazalendo Omar Shaaban, mgombea ubunge wa Temeke Sheikh Ponda Issa Ponda, na Naibu Katibu wa Uenezi Taifa Shangwe Ayo.


Kurejeshwa kwa fomu hizo kunafuatia uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma uliotolewa Septemba 11, 2025, ambapo majaji walibatilisha zuio lililomnyima nafasi awali, wakibainisha kuwa mchakato uliotumika haukuwa halali kisheria. Uamuzi huo ulimfungulia njia Mpina kuendelea na mchakato kama wagombea wengine.


Kwa hatua hiyo, Mpina sasa anakuwa miongoni mwa wagombea urais watakaowania nafasi ya juu kabisa ya uongozi nchini katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.


Post a Comment

0 Comments